Monday, April 8, 2013

KESI YA VIGOGO WA CHADEMA KUNGURUMA LEO SINGIDA

Mshitakiwa wa kwanza katika kesi ya kumtolea lugha ya matusi mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi Mwita Waitara Mwakibe akitoka nje ya mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida

Kesi  inayowakabili vigogo wawili wa CHADEMA kwa tuhuma ya kumtolea lugha ya matusi mbunge wa jimbo la Iramba magharibi Mh. Lameck Mwigullu, inatarajiwa kuunguruma leo asubuhi kwenye mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida.
Kesi hiyo imeshindwa kuendelea kusikilizwa mara mbili baada ya
mashahidi  wa upande wa mashitaka kushindwa kufika mahakamani.
Baada ya mashahidi hao wa upande wa mashitaka kushindwa kufika mahakamani na hakimu anayeisikiliza kesi hiyo Flora Ndale, aliagiza kuwa juhudi zifanyike ili kuhakikisha kuwa mashahidi hao wanafika mahakamani hapo, Aprili nane mwaka huu bila kukosa ili waweze kutoa ushahidi wao.
Hakimu Ndale amesema kuwa kitendo cha mashahidi wa upande wa mashitaka kutokufika mahakamani wakati washitakiwa kutoka Dar-es-salaam, wanafika mahakamani hapo kila tarehe ya kesi ni usumbufu mkubwa kwa washitakiwa,mawakili wao na wasikilizaji.
Vigogo hao ambao wanatuhumiwa kumtolea lugha ya matusi mbunge wa jimbo la Iramba magharibi Mh. Mwigulu Chemba ni Waitara Mwikwabe (37) Afisa Sera na Utafiti makao makuu na Dk.Kitila Mkumbo Mhadhiri wa chuo kikuu Dar-es-salaam na mshauri  wa CHADEMA.
Vigogo hao wanatuhumiwa kutenda kosa hilo Julai 14 mwaka huu saa kumi jioni.
Kwa mujiubu wa mwanasheria wa serikali Seif Ahmed, washitakiwa bila halali, walimtusi mbunge Mwigullu kuwa ni malaya, mzinzi na mpumbavu huku wakijuwa wazi kuwa kitendo hicho ni kinyume na sheria.
Seif amesema kuwa washitakiwa hao bila halali, alitenda kosa hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Nguvumali kwa lengo la viongozi wa CHADEMA kuzungumza na wananchi.

No comments:

Post a Comment