Saturday, April 13, 2013

Wakazi wa Utemini Singida wailalamikia manispaa kwa kutekelekeza barabara na kuzifanya kugeuka makorongo ya maji.



Barabara ya kuanzia klabu cha pombe za kienyeji cha Bulongwa kilichopo eneo la Utemini Singida mjini ikiwa imegeuka mto na kusababisha magari kushindwa kupita.

Wakazi  wa mtaa wa Utemini stesheni  Singida mjini wameilalamikia halmashauri ya manispaa ya Singida, kwa kitendo chake cha kuzitelekeza barabara za eneo hilo na kusababisha zigeuke kuwa mito yenye makorogo makubwa.
Wamedai kuwa mito na makorogo hayo yanatishia usalama wao kwa kiwango kuikubwa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wamedai kuwa barabara ya kuanzia
klabu ya pombe za kienyeji ya Bulongwa hadi nyumbani kwa Dk.Kiunsi, imegeuka kuwa mto wenye makorongo makubwa na yenye kina kirefu.
Moja wa wakazi hao Juma Kidimanda amesema licha ya kwamba maji ya mvua ya mto huo yanaweza kusomba mtu/watu, pia inawawia vigumu watu wanaouguliwa na wale wenye wajawazito kusafirisha ndugu zao hao kuwapeleka hospitali.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Utemini Baltazari Kimario amekiri kuharibika kwa barabara hiyo, lakini akadai kuwa hivi sasa TAMISEMI imeahidi kuitengeneza kwa fedha zake.
Akifafanua, amesema maafisa wa TAMISEMI wameshaikagua barabara hiyo na kuahidi kuigharamia matengenezo yake pamoja na kuchimba mirefeji kwa pande zote mbili.

1 comment:

  1. AnonymousMay 01, 2013

    Ndugu tunaomba picha nzuri nzuri za mjini Singida ili ipate kujulikana na watu wa nje wanafatilia mtandao wako itakua vizuri hivyo unatangazia mji wako.

    ReplyDelete