Wednesday, April 10, 2013

Mtoto wa mwezi mmoja kuuawa na mama yake mzazi kwa kukatwa na panga kichwani,Singida.


 


                                                 PICHA ZOTE KUTOKA MAKTABA

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP Linus Sinzumwa, amesema mtoto Halawa Msika mkazi wa kijiji cha Lugongo kata na tarafa ya Ibaga, aliuawa na mama yake mzazi Njile Makelemo (40) kwa kumkatakata kichwani kwa panga na kusababisha kifo chake papo hapo.
Amesema tukio hilo la kusikitisha limetokea Aprili mosi mwaka huu saa tatu usiku huko katika kijiji cha Lugongo wilaya mpya ya Mkalama.
Sinzumwa amesema pia mama huyo anayedaiwa kuwa na matatizo ya akili, aliwajeruhi watoto wake wengine Jandika Msika (2)  na Hoga Msika (17) wote kwa kuwakatwa panga katika mikono yao yote miwili.
Kamanda huyo amesema hivi sasa watoto hao wawili wamelazwa katika hospitali ya misheni  Iyambi na hali zao sio nzuri.
Amesema upelelezi wa awali umebaini kwamba mtuhumiwa huyo ana matatizo ya akili na tayari ameisha kamatwa na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote upelelezi utakapo kamilika.

No comments:

Post a Comment