Wednesday, April 10, 2013

VIKUNDI VYA KWAYA SINGIDA VYATAKIWA KULENGA KUIELIMISHA JAMII KUISHI MAISHA YA UADILIFU.


Kwaya ya Rivaivo inayomilkiwa na kanisa la Free Pentekoste Church la mjini Singida ikitoa burudani na kuelimisha wakati wa ibada ya Jumapili kanisa hapo.

Askofu wa kanisa la Free Pentekoste Church (FPCT) mkoani Singida Paulo Samwel amevitaka vikundi vya kwaya za injili, kujiwekea malengo ya kutoa huduma ya nyimbo za injili ndani na nje ya nchi.
Askofu Samweli ametoa changamoto hiyo wakati akitoa nasaha zake kwenye hafla iliyofana ya mazoezi ya kwaya ya Revaivoya mjini Singida, ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kurekodi kanda yake ya DVD.
Amesema uzoefu unaonyesha wazi kuwa vikundi vya kwaya, vinafanya kazi nzuri ambazo ni pamoja na kuwahimiza na kuwahamasisha waumini kumcha Mungu na wakati huo huo, kuielimisha jamii kuishi maisha ya uadlifu kama njia mojawapo ya kudumisha amani na utulivu.
Ameisema vikundi vya kwaya pamoja na kutoa huduma nzuri kwa waumini, lakini pia
vina wajibu wa kuihudumia jamii nyingine katika kuielimisha juu ya umuhimu wa kuishi maisha ya uadilifu na kufanya kazi halali kwa bidii ili kuboresha hali zao kiuchumi.
Kwa hali hiyo, Askofu Samwel amesema kutokana na umuhimu huo, vikundi vinapaswa kutoa huduma yao ndani na nje ya nchi, ili iweze kuwafikia watu wengi zaidi wenye tamaduni tofauti tofauti.

No comments:

Post a Comment