Monday, November 19, 2012

KESI YA VIGOGO WA CHADEMA KUMTUSI MBUNGE WA IRAMBA ILIYOKUWA ISIKILIZWE LEO YAAHIRISHWA HADI DESEMBA 17 MWAKA HUU.

Mhadhiri wa chuo kikuu Dar-es-salaam, Dk.Kitila Mkumbo (kushoto) akitetea jambo na wakili wake Raymond Kimu muda mfupi kabla hajasomewa shitaka lake la kutoa lugha ya matusi kwa mbunge wa jimbo la Iramba magharibi Mwigullu Nchemba.


Kesi inayowakabili vigogo wawili wa CHADEMA taifa, imeaahirishwa hadi Desemba 17 mwaka huu kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutokana na mwanasheria wa serikali kuugua.
Imeelezwa mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi Ruth Massamu, kuwa mwanasheria huyo wa serikali Maria Mdulugu anayesimamia kesi hiyo ni mgonjwa.
Vigogo hao ambao wanatuhumiwa kumtolea lugha ya matusi mbunge wa jimbo la Iramba magharibi Mh. Mwigulu NChemba ni Afisa Sera na Utafiti makao makuu Waitara Mwikwabe (37) na Mhadhiri wa chuo kikuu Dar-es-salaam na mshauri  wa CHADEMA Dkt. Kitila Mkumbo.
Kwa mujiubu wa mwanasheria wa serikali Seif Ahmed, washitakiwa bila halali, walimtusi mbunge Mwigullu kuwa ni malaya, mzinzi na mpumbavu huku akijuwa wazi kuwa kitendo hicho ni kinyume na sheria.
Seif amesema kuwa washitakiwa hao bila halali, walitenda kosa hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Nguvumali kwa lengo la viongozi wa CHADEMA kuzungumza na wananchi.

No comments:

Post a Comment