Friday, October 25, 2013

MSAKO MAALUM KWA WANAOISHI KINYUME NA SHERIA MKOANI SINGIDA


PICHA ZOTE NI KUTOKA MAKTABA YA SINGIDAYETUBLOG

Mkoa wa singida unatarajia kuanza operation ya ukaguzi wa kubaini watu wanaoishi nchini kinyume na sheria.
Hayo yamebainishwa jana na Afisa uhamiaji mkoa wa Singida Bw. Adam Mnyeke wakati akizungumza katika siku maalum ya polisi iliyofanyika katika ukumbi wa Aquar Manispaa ya Singida,
Bw. Mnyeke amesema kuwa zoezi hilo linatarajia kuanza wiki ijayo, hivyo kutoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa taasisi hiyo ili kupambana na wahamiaji haramu.
Amesema kwa kuanza, zoezi hilo litaanzia manispaa ya singida na baadaye litakwenda katika wilaya nyingine za mkoa wa Singida, na kuongeza kuwa zoezi hilo pia litasaidia kupambana na vitendo vya uhalifu ambavyo mara nyingi vimekuwa vikifanywa na wahamiaji haramu.

No comments:

Post a Comment