Monday, October 14, 2013

ONGEZEKO LA WATU KATIKA MJI WA SINGIDA WAONGEZA UZALISHAJI WA TAKA.

                                                     (Picha zote kutoka maktaba)

Kuongezeka kwa idadi ya watu katika kata ya Mandewa Manispaa ya Singida kumesababisha kuongezeka kwa uzalishaji wa taka laini na ngumu katika kata hiyo na maeneo jirani.

Mwenyekiti wa kamati ya usafi na mazingira kata ya Mandewa Bw. Elifuraha Mgoma amesema hayo muda mfupi baada ya kumaliza shughuli za kufanya usafi eneo la Ginery manispaa ya Singida.

Amesema hivi sasa kunaongezeko watu lilochangiwa na taasisi za elimu kama vile vyuo, pamoja na shule jambo ambalo limepelekea kuongezeka kwa wingi wa uzalishaji wa taka katika maeneo ambayo watu hao wanaishi.

Amesema jitihada za haraka zinahitajika ili kukabiliana na tatizo hilo ikiwa ni pamoja na kujenga guba la kukusanyia uchafu kwa lengo la kuepukana magonjwa ya miripuko yanayoweza kutokea kwa sababu ya kuzagaa kwa taka

No comments:

Post a Comment