Tuesday, October 8, 2013

Kampuni ya madini ya Shanta yatumia shilingi 23.6 milioni kugharamia ujenzi wa matundu ya choo

 Mkuu wa wilaya ya Ikungi,Manju Msambya, akizungumza kwenye mahafali ya 48 ya shule ya msingi ya Mang’onyi.Wa kwanza kushoto ni meneja mahusiano wa kampuni ya madini ya Shanta na anayefuatia ni mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi ya Mang’onyi, Andrea Andalu.
 Mkuu wa wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida,Manju Msambya (wa pili kulia) akikata utepe kuzindua choo chenye matundu 40 cha shule ya msingi Mang’onyi kilichojengwa na kampuni ya Shanta.Wa kwanza kulia ni afisa elimu wilaya ya Ikungi Gerald Kivuyo.Wa kwanza kushoto ni meneja mahusinao wa kampuni ya madini ya Shanta,Credo Simbaye na anayefuata ni mkuu wa shule ya msingi ya Mang’onyi, Adamu Mwekwa.
 Mkuu wa wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Manju Msambya akigawa vyeti kwa mmoja wa wahitimu wa darasa la saba wa shule hiyo.
 Jengo la ofisi ya kijiji cha Mang’onyi kilichojengwa kwa msaada ya kampuni ya madini ya Shanta.
 Jengo la kituo cha kisasa cha polisi kata ya Mang’onyi kinachoendelea kujengwa kwa msaada ana kampuni ya madini ya Shanta.Anayeonyesha jengo hilo la kituo cha polisi,ni meneja Ardhi na Makazi wa kampuni ya madini, Elisante Kamuya.
              Vyumba vya Choo vilivyojengwa na Kampuni ya madini ya Shanta.
Jengo la choo cha shule ya msingi cha zamani cha shule ya msingi Mang’onyi wilaya ya Ikungi ambacho hakifai kwa matumizi tena.

Kampuni ya madini ya Shanta Singida imetumia zaidi ya shilingi 23.6 milioni kugharamia ujenzi wa choo cha matundu 40 katika shule ya msingi Mang’onyi jimbo la Singida mashariki.

Hayo yamesemwa juzi na Meneja Mahusiano wa kampuni ya madini Shanta,Credo Simbaye wakati akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano ya choo hicho iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Mang’onyi.

Amesema kwamba uamuzi wa kampuni ya Shanta kutoa msaada huo wa ujenzi wa choo ni kuinusuru shule hiyo kufungwa kutokana na kukosa choo.

“Baada ya mamlaka husika kutaka kuifunga shule hii kongwe kwa muda usiojulika kutokana na kukosa kabisa choo kamati ya shule ilileta ombi kwetu tusaidie kuijengea choo cha matundu 40 ili isifungwe na wanafunzi zaidi ya elfu moja wakakosa masomo ombi hilo tulilipokea kwa mikono miwili”,alisema Simbeya

Meneja Mahusiano huyo amesema pamoja na Shanta bado haijaanza shughuli zake za uchimbaji madini iliona upo umuhimu mkubwa kujenga choo kwa shule hiyo ili wanafunzi wasikatishe masomo kwa tatizo la choo.

“Unapowekeza  katika biashara ya madini au maliasili yo yote ile kimsingi unakuwa umekubali pia kuwa mdau wa maendeleo ya wananchi katika eneo husikajukumu mojawapo ni kuhakikisha kwamba msukumo wa maendeleo yanayotarajiwa unapata nguvu za pamoja”amesema Simbaye.

Aidha amesema pia hivi sasa wapo kwenye maandalizi ya
kuchimba kisima kirefu cha maji kitakachosaidia kupunguza uhaba mkubwa wa maji unaochangia wakazi wa kata ya Mang’onyi kuchangia maji na mifugo.

“Kama nilivyosema awali kwamba Shanta haijaanza kuchimba madini lakini hilo halijazuia kampuni kutoa misaada ili kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa kata ya Mang’onyi.

Simbaye amesema kwa sasa wanajenga chumba cha darasa katika shule ya msingi Mlumba kituo cha kisasa cha polisi kata ya Mang’onyi,vijana 210 wamepata ajira za muda na kampuni imeendelea kutoa magari kwa ajili ya kusafirisha wagonjwa kuwapeleka kituo cha afya Ikungi na zahanati ya kijiji cha Mwau.


“Wito wangu kwa wananchi wa wilaya ya Ikungi na hususan wa kata ya Mang’onyi ,nawaomba waamini kwamba,mradi wa dhahabu wa Shanta Singida,utakapoanza utafungua ukurasa mpya wa maendeleo kwa wilaya ya Ikungi na mkoa wa Singida,hivyo hawana budi kuunga mkono”,alisema meneja Simbaye.

1 comment:

  1. Prosper hilary(puma)October 08, 2013

    Nikitu kizuri nimeipenda,sio wanachimba wanatuachia mashimo,

    ReplyDelete