Thursday, January 30, 2014

Nyalandu apongezwa na wapiga kura wake.

Waziri Maliasili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akisalimiana na mwenyekiti mstaafu wa CCM wilaya ya Singida, Swalehe Msuri katika viwanja vya Mtinko jimbo la Singida Kaskazini.Waziri Nyalandu alikuwa Mtinko kuhudhuria hafla ya kupongewa kuwa waziri kamili wa Maliasili na Utalii.
Waziri Maliasili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akikabidhiwa mkuki na mzee Ntandu ili akautumie katika kupambana na ujangili.Nyalandu alikabidhiwa mkuki huo kwenye hafla ya kumpongeza iliyofanyika katika kijiji cha Mtinko kwa kuteuliwa kuwa Waziri Maliasili na Utalli.
Waziri Maliasli na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akizungumza kwenye hafla ya kupongezwa na wapiga kuwa wake wa jimbo la Singida Kaskazini kwa kuteuliwa kuwa waziri kamili wa Wizara hiyo ya Maliasili na Utalii.Hafla hiyo iliyofana,ilifanyikia kwenye viwanja vya ofisi ya kijiji cha Mtinko.
Baadhi ya viongozi wilaya ya Singida waliohudhuria halfa ya kumpongeza Mh. Lazaro Nyalandu kwa kuteuliwa kuwa Waziri Maliasli na Utalli.Hafla hiyo iliyofana ilifanyikia katika kijiji cha Mtinko jimbo la Singida kaskazini.
Baadhi ya wananchi wa jimbo la Singida kaskazini waliohudhuria hafla ya Waziri Maliasili na Utalii, Mh.Lazaro Nyalandu kwa kuteuliwa kuongoza wizara hiyo.

No comments:

Post a Comment