Tuesday, November 20, 2012

MARTHA MLATA AENDESHA HARAMBEE YA KUCHANGIA UJENZI WA MSIKITI SINGIDA.

 Mbunge wa viti maalum (CCM) mkoa wa Singida,Martha Mlata (wa pili kushoto) akipokelewa na waumini wa msikiti wa Almasijidi Muhidini Baytulah wa kitongoji cha Mbuyu Senene kijiji cha Iguguno wilaya ya Mkalama,akipokelewa na waumini wa msikiti huo.
 Imamu wa msikiti wa Nuru Salama Unyankindi mjini Singida,Yahaya Mahiki akitoa nasaha zake kwenye hafla ya harambee ya kuchangia kumalizia ujenzi wa msikiti wa Almasijidi Muhidini Baytulah wa kitongoji cha Mbuyu Senene kijiji cha Iguguno wilaya ya Mkalama.

  Mbunge wa viti maalum (CCM) mkoa wa Singida Martha Mlata akihutubia waumini wa kiislamu wa kijiji cha Igiguno wilaya ya Mkalama juzi waliohudhuria hafla ya harambee ya kuchangia umalizaji wa msikiti wa Almasijidi Muhidin Baytuhal.Kulia ni katibu wa wananwake wa msikiti huo Mama Mariamu na kushoto ni diwani wa kata ya Iguguno Bi Lyochi.
Baadhi ya waumini wa kiislamu waliohudhuria hafla ya kuchangia umalizaji wa msikiti wa Almasijidi Muhidin Baytuhal wa kitongoji cha Mbuyu Seenene wilaya ya Mkalama.Harambee hiyo ilikusanya zaidi ya shilingi milioni nne ambazo ni fedha taslimu na ahadi.

No comments:

Post a Comment