Saturday, January 12, 2013

Mgana Msindai awataka madereva Singida kutii sheria bila shurti kuepukana na usumbufu.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida,Mgana Msindai (mwenye kofia ya tunga) akikabidhiwa zawadi ya mbuzi mbili na viongozi wa umoja wa mabasi madogo (Hiace) mjini Singida.Umoja huo umetoa zawadi hiyo kwa kitendo cha mwenyekiti huyo kufanikisha mabasi madogo yaanze kutumia kituo cha zamani cha mabasi mjini Singida.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida Mgana Msindai amewahimiza madereva wa vyombo vya moto yakiwemo mabasi madogo kutii sheria bila shurti, ili kuepuekana na usumbufu unaochangia kupoteza muda mwingi.
Msindai ametoa wito huo wakati akizungumza na viongozi wa umoja wa madereva wa mabasi madogo (hiece) yanayofanya safari kati ya
Singida mjini na Igunga mkoani Tabora na Singida mjini hadi Ilongero Singida vijijni.
Amesema uzoefu unaonyesha wazi kuwa madereva wengi na hasa wa bodaboda na mabasi makubwa na madogo, huvunja sheria zilizowekwa kwa makusudi lengo likuwa ni kuwahi abiria.
Msindai amesema kitendo hicho hupelekea wakamatwe na polisi na kisha kutozwa faini za papo kwa papo au kufikishwa mahakamani ambapo hupoteza muda mwingi ambao angeutumia kujiingizia mapato.
Kuhusu mabasi madogo kuruhusiwa kutumia kituo cha mabasi cha zamani, Msindai amesema mabasi madogo yameruhusiwa kutumia kituo hicho kwa muda wakati manispaa ikiendelea kutafuta mwekezaji wa kujenga kitega uchumi.

No comments:

Post a Comment