Saturday, January 26, 2013

Wanafunzi mkoani Singida watakiwa kujenga utamaduni wa kupanda miti katika makazi yao

 Mkuu wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Kone akishiriki kupanda miti katika siku ya uzinduzi wa miti ki-mkoa.Uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya shule ya sekondari ya Unyamikumbi manispaa ya Singida.
 Naibu meya wa manispaa ya Singida, Shaban Mkata akishiriki kupanda mti kwenye uzinduzi wa upandaji miti ki mkoa uliofanyika katika shule ya sekondari ya Unyamikumbi manispaa ya Singida.

Diwani wa viti maalum Mama Alute akipanda mti kwenye uzinduzi wa upandaji miti kimkoa.
 Baadhi ya wakazi wa kata ya Kisaki manispaa ya Singida na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Unyamikumbi wakimsikiliza kwa makini mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone (hayupo kwenye picha) akizungumza kwenye hafla ya upandaji miti ki-mkoa.

Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone amewaagiza wanafunzi kujenga utamaduni wa kupanda miti miwili katika makazi yao kila mwaka na kuitunza na kuilinda vizuri ili iweze kukua.
 Dkt.Kone ametoa wito huo wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa upandaji miti ki-mkoa,uliofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari ya kata ya Unyamikumbi manispaa ya Singida.
 Amesema kijana akijenga utamaduni wa kupanda miti na kuitunza vizuri, kwanza atakuwa
anaipenda na kuithamini miti na kwa njia hiyo, atahakikisha miti haivunwi hovyo kitendo kitakachochangia mkoa kutokugeuka jangwa.
Dtk. Kone amewataka kuwa na utamaduni huo wa kupanda miti miwili moja ukiwa wa matunda, uendelezwe hadi katika shule na vyuo watakapo bahatika kupitia.
 Amesema endapo wanafunzi kila mmoja atatekeleza agizo hilo kwa makini, watakuwa wameshiriki vyema katika mapambano dhidi ya mkoa na nchi kugeuka jangwa.

No comments:

Post a Comment