Thursday, January 10, 2013

Mkoa wa Singida wafanikiwa kupunguza idadi ya vifo vya kina mama wajawazito na watoto hadi kufikia 85 kwa kila laki moja.

            Sehemu ya hospitali ya rufaa ya mkoa wa Singida inayoendelea kujengwa hivi sasa.

Mkoa wa Singida umetumia zaidi ya shilingi bilioni 6.1 kugharamia ujenzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa katika kipindi cha kuanzia mwaka 2009 hadi mwaka jana.
Mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone amebainisha hayo wakati akitoa taarifa yake ya utekelezaji wa
ilani ya uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha mwaka 2005 hadi mwaka jana.
Amesema fedha hizo zimetumika kugharamia ujenzi wa majengo mawili ya wagonjwa wa nje (OPD) na  jengo la wazazi ambayo tayari yamekamilika.
Dkt. Kone amesema pia fedha hizo zimetumika katika ujenzi wa awamu ya pili ya mradi huo kwa kujenga jengo la utambuzi wa magonjwa ambalo limekamilika kwa asilimia 95.
Amesema kwa mwaka huu wa fedha wa 2012/2013, serikali kuu imewatengea shilingi bilioni 1,805,154,000 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa hospitali ya rufaa.
Kuhusu vifo vya akina mama wajawazito, mkuu huyo amesema vifo hivyo vinavyotokana na uzazi, vimepungua kutoka 233/100,000 vya mwaka 2005, hadi vifo 87/100,000 kwa kila vizazi hai juu mwaka jana.
Mkuu huyo wa mko amesema mafanikio hayo yametokana na kuongezeka kwa idadi ya akina mama wajawazito  kujifungulia katika vituo vya afya.

No comments:

Post a Comment