Friday, November 16, 2012

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SINGIDA LAMTOLEA UVIVU MHANDISI MASORO NA KUTAMKA KUWA HALIMTAKI TENA.

 Mstahiki meya wa manispaa ya Singida Sheikh Salum Mahami (katikati) akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani Mkoani Singida.
Pantaleo Sorongai, Diwani wa Mitunduruni akimlalamikia mhandisi wa manispaa Singida Robart Massoro kutokana na utendaji mbovu wa kazi zake


Baraza la madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Singida limetoa tamko rasmi kwamba halimhitaji tena mhandisi wa ujenzi Robert Masoro, kwa madai kwamba utendaji wake haukidhi  matarajio ya wakazi wa manispaa hiyo.
Tamko hilo limetolewa na mstahiki meya wa manispaa ya Singida Sheikh Salum Mahami, mbele ya kikao cha baraza la madwaini, kilichofanyikia kwenye ukumbi wa mikutnao wa FDC mjini Singida.
Mapema wakati baraza hilo linaendelea, yalitokea malalamiko mengi kutoka kwa madiwani kwamba kazi nyingi zinazosimamiwa na mhandisi Masoro, zimekuwa chini ya kiwango, kitendo walichodai kuwa  manispaa hiyo inaingia hasara kubwa.
Imedaiwa zaidi kwamba kazi anazozisimamia mhandisi huyo, zikiwemo za ujenzi wa barabara, zimekuwa hazifanani na thamani ya fedha zilizotumika.
Baada ya kumaliza kikao hicho cha kamati ambacho kilichukua zaidi ya saa moja na nusu, ndipo Meya sheikh Mahami alipotoa tamko hilo.
Sheikh Mahami ambaye pia ni Sheikh wa mkoa wa Singida, amesema mhandisi Masoro pamoja na mambo mengine, amekuwa na manyanyaso ya wazi wazi dhidi ya makandarasi.
Mhandisi Masoro amekuwa akikumbwa na misuko suko mingi katika utendaji wake wa kazi.
Hivi karibuni kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka huu, Kapteni Honest alikosoa miradi yote iliyiosimamiwa na mhandisi Masoro na kuahidi kuchukua jina lake na kulipeleka katika ngazi za juu kwa maamuzi zaidi.

No comments:

Post a Comment